Ijumaa, 30 Juni 2017

Rudisha nguvu za kiume zilizopotea

Namna ya kurudisha nguvu za kiume zilizopotea kwasababu ya kuongezeka unene

    Kupoteza au kupungukiwa nguvu za kiume ni hali ya mwanaume kushindwa kusimamisha uume, uume kusimama kilegevu, kupoteza hamu ya tendo la ndoa baada ya kufika kileleni Mara moja, uume kushindwa kusimama hadi unapofika kileleni au kukosa hamu ya kufanya tendon la ndoa. Hali hii huwapata wanaume wengi wa rika zote ingawa ni tatizo zaidi kwa wanaume walio na umri wa miaka 50 na kuendelea.

    Zipo sababu nyingi zinazoweza kusababisha mwanaume kupungukiwa nguvu za kiume, hapa tutaangalia tatizo la unene linavyoweza kusababisha tatizo na namna ya kulitibu.
   Unene huweza kupelekea matatizo ya msukumo wa damu ambayo hufanya kupungua kwa kiwango cha damu inayojaa katika misuli ya uume, jambo hili huweza kupelekea nguvu za kiume kupungua au kuimengi
 

 Namna ya kutibu tatizo

   Ili kurejesha nguvu zako za kiume unapasa kufanya yafuatayo
Fanya jitihada za kupunguza unene na uzito wako uliozidi. Zipo njia mbalimbali za kupunguza unene ikiwepo kufanya mazoezi yakutosha, kutengeneza aina ya mlo utakaopunguza unene ndani ya muda mfupi pamoja na nyinginezo. Yako masomo mengine yanayo kufundisha namna ya kufanya ili kupunguza unene.
Kunywa maji mengi na kula matikitiki maji kwa wingi ili kusafisha mfumo wa mzunguko wa damu.

Kula matunda na mboga za majani kwa wingi kuliko vyakula vya nyama na wanga.
Kula kwa wingi vyakula kama mbegu za maboga, karanga, nazi na jamii zake.
Tumia vitunguu swaumu marambili kwa Siku, chukua vipande sita hadi nane vya kitunguu swaumu, vimenye kisha uvikatekate katika vipande vidogovidogo kisha uvinywe kama vidonge, Fanya zoezi hilo kwa mwezi mmoja.


 

Jumatano, 3 Mei 2017

Yajue magonjwa ya fangasi ya ngozi na matibabu yake

Magonjwa ya fangasi ya ngozi na matibabu yake

      Fangasi ni magonjwa yanayoathiri ngozi, kucha na nywele, pia huathiri mdomoni na ukeni. Magonjwa haya huambukiza kwa njia ya kugusana ua kshirikiana nguo hasa za ndani na tauro.

      Hapa tutaangalia fangasi katika kundi la magonjwa yanayoathiri ngozi, nywele na kucha (dermatomycosis).

      Kuna aina kuu 5 za magonjwa ya fangasi wa ngozi, nywele na kucha kama ifuatavyo;


  • Fangasi wa kichwani, ugonjwa huu huanza na sehemu ndogo ya ngozi ya kichwa na kukua kuwa sehemu kubwa. Huathiri nywele na kuzifanya dhaifu, laini na nyepesi kukatika au kung'oka. Huwaathiri sana watoti chini ya miaka 10 na hupotea mtu akisha barehe. Matibabu take  ni  griseofulvin na fluconazole, dozi zake huanzia siku 6-14.



  • Fangasi wa mwili, ugonjwa huu hutokea mwilini, sehemu ya ngozi iliyoathiriwa huwa nyekundu, duara kama shiringi na kukua huku ikiacha sehemu ya katikati kuwa na ngozi nzuri. Maduara haya yanaweza kukaa yakiwa kadhaa katika sehemu moja ya ngozi. Dawa nzuri kutumia ni za kupaka zinazokuwa katika tyubu, cotrimazole au ketoconazole. Kwa ugonjwa uliokua sana na kwa wagonjwa wenye kinga ya mwili ndogo kama wenye VVU, nivema wakatumia dawa ya kunywa




  • Fangasi wa nyayo na vidole, ugonjwa huu hutokea kama mabaka na kuchanika katikati ya vidole na huwacha sana na kuuma pia. Matibabu yake maranyingi huwa dawa ya kupaka kwa wiki 4, kwa ugonjwa uliokua sana tumia dawa ya kunywa kama griseofulvin kwa wiki 6-12.



  • Fangasi wa kucha, ugonjwa huu huathiri kucha na hubadilisha rangi ya kucha. Huzalishwa vitu kama chaki na ambavyo vikisuguliwa huweza kupukutika. Kucha huweza kulika na inaweza kuisha. Ili kutibu ugonjwa huu nibora kutumia dawa za kunjwa na terbinafine na itraconazole zimeonekana dawa bora zaidi.



  • Pityriasis, huu ni ugonjwa wa fangasi ambao huathiri sehemu ya huu sana ya ngozi katika sehemu za usoni, shingoni na mgongoni. Hutokea kama viduara vyenye mng'ao vinavyo washa. Huongezeka na huathiri sehemu kubwa ya ngozi visipotibiwa ingwa vinaweza kupotea vyenyewe. Maranyingi ugonjwa huu hauambukizwi Ila hutokea kama ajari tu yaapotikea mabadiliko fulani ya mwili. Sio ugonjwa hari sana kiafya ila haukubaliki kwani huharibu mwonekano wa mtu has a unapotokea maeneo ya uso na shingoni. Matibabu yake ni sawa na yale ya fangasi wa mwili.

Jumamosi, 29 Aprili 2017

Jua ugonjwa wa kuoza fizi na namna ya kuuzuwia na kuutibu

Ugonjwa wa kuoza fizi

   Ugonjwa wa kuoza fizi ni ugonjwa unaotokea Mara chache na hutokea zaidi katika nchi zinazoendelea Kama Tanzania hasa katika maeneo ya watu maskini. Ugonjwa huwa hatari ikiwa utaendelea sana na kusababisha fizi kuozasana has a pale unapopelekea maambukizi ya magonjwa mengine.

Mambo yanayoweza kupelekea  ugonjwa huu

  • Kinywa kichafu, uchafu wa kinywa hupelekea kukua kwa bacteria hatari wanaoweza kupelekea ugonjwa.
  • Uvutaji sigara na matumizi ya ugoro na kubeli yanaweza kupelekea tatizo.
  • Afya mgogoro, mtu mwenye afya mgogoro anaweza kupelekea bacteria walio kinywani wasio na madhara kupelekea madhara na kusababisha ugonjwa.
  • Msongo wa mawazo
  • Kinga ya mwili kushuka kutokana sababu mbalimbali ukiwemo UKIMWI au magonjwa sugu kama kisukari.
  • Maambukizi ya magonjwa ya kinywa

Dalili za ugonjwa

Harufu mbaya ya kutoka kinywani na kuhisi radha mbaya
  • Damu kuvuja katika fizi kwa urahisi
  • Vidonda katika fizi
  • Kuvimba fizi na kuwa njekundu
  • Fizi kuuma
  • Fizi koza na kupukutika
  • Fizi kutokwa usaha

Matibabu 

Unapoona dalili za namna hii hapo juu, nivema uende hospitality ili ukaonane na daktari wa kinywa na meno, ikiwa unashindwa kuhospitali, fanya yafuatayo
  • Safisha kinywa chako kwa maji na kitambaa safi na laini
  • Nunua dawa ya kusukutua kinywani ( chlorhexidine ), sukutua kinywa chako kwa kufuata maelekezo utakayopewa unapoinunua.
  • Tumia amoxicycilne na paracetamol endapo unahisi msumivu ya fizi au homa, unaweza kiongeza metronidazole (frajiri) endapo tatizo ni kubwa. Tumia dozi ya Sikh tank kwa hili dawa isipokuwa paracetamol ambayo unaweza kutumia kwa Siku 3, hakikisha unafuata maelekezo ya matumizi ya dawa hizo uliyopewa wakati unazinunua.

Namna ya kukinga ugonjwa

Hakikisha unafanya usafi wa kinywa chako na kutembelea kliniki ya kinywa na meno walau Mara 2 kwa mwaka ili kupata ushauri, kukinga na kutibu magonjwa nyemerezi ya kinywa na meno.


Jumamosi, 22 Aprili 2017

Jua namna ya kumsaidia mtu aliepata mshituko

Ujue mshituko na namna ya kumsaidia mtu aliyepatwa na mshituko (Shock)


      Mshituko ni tatizo la kiafya linalompata mtu kutokana na kupungua kwa damu katika ubongo au kuathiliwa kwa mfumo wa fahamu. Tatizo hili linaweza kumpata mtu wa jinsia yoyote na umri wowote.

      Zipo aina tano za mshituko kama ifuatavyo;

  •   Mshituko unaosababishwa na  matatizo ya moyo
  • Mshituko unaoshababishwa na upungufu wa damu
  • Mshituko unaosababishwa na maambukizi ya damu 
  • Mshituko unaosababishwa na aleji
  • Mshituko unaosababishwa na kuathiriwa kwa mfumo wa fahamu


   Mshituko unaosababishwa na moyo

       Moyo unaweza kushindwa kusukuma damu katika baadhi ya viungo kama ubongo na kupelekea kupungua kwa oksijeni katika ubongo, jambo hili linaweza kupelekea mshituko.
Moyo unaweza kushindwa kusukuma damu ipasavyo kutokana na magonjwa ya moyo.

Mshituko unaosababishwa na kupungua kwa damu

      Kupungua kwa damu katika mzunguko wake hupelekea kupungua
kwa kiwango cha damu inayosukumwa kuenda katika ubongo na kupelekea mshituko.
       Kupungua kwa damu katika mzunguko wake kunaweza kusababishwa na mambo yafuatayo;

  • Kujeruhiwa na kuvuja damu nyingi
  • Kuungua
  • Kuharisha
  • Maji kukimbilia sehemu za wazi za mwili kama zile zinazozunguka mapafu na tumbo

Mshituko unaosababishwa na maambukizi ya damu

      Hii hutokea pale bacteria wanapoingia katika damu na kumsikumo sumu. Sumu hii inapokua katika damu husababisha kulegea na kutanuka kwa mishipa ya damu. Mishipa ikitanuka hupunguza msukumo wa damu na kupelekea damu kushindwa kufika sehemu za juu za mwili hasa katika ubongo, jambo hili huweza kusababisha mshituko.

Mshituko unaosababishwa na aleji

      Hii hutokea pale chemikali toka nje ya mwili zinaposhindana na mwili na kusababisha kulegea na kutanuka kwa mishipa ya damu. Hali hii kupelekea kupungua msukumo wa damu na kufanya upungufu wa damu kufika katika ubongo na kupelekea mshituko.

Mshituko unaosababishwa na kuathiriwa kwa mfumo wa fahamu

      Hii hutokea pale mtu anapopata msongo wa mawazo au uwoga, mfumo wa fahamu huweza kuathirika na kupelekea mshituko.

Dalili za mshituko


  • Ngozi baridi iliyopauka isipokuwa kwa mshituko unaosababishwa na maambukizi ya damu ambayo ngozi huwa yenye joto
  • Kuchanganyikiwa akili na kukosa utulivu
  • Kutokwa na jasho
  • Kutokupata mkojo
  • Kubadilika rangi na kuwa mweupe rangi inanyoonesha upungufu wa damu
  • Mgonjwa anaweza kupoteza fahamu
  • Pumzi ya chini na ya harakaharaka na mapigo ya moyo kuwa ya harakaharaka


Namna ya kumsaidia mgonjwa


  • Mweke mgonjwa katika sehemu yenye hewa safi na yakutosha
  • Regeza nguo za mwili wake
  • Mlaze mgonjwa chali na kichwa chake kikitazama upande kuruhusu mate kutokana nje ili asipakiwe, hii ni kwa mgonjwa alipoteza fahamu
  • Mlaze miguu yake ikiwa juu kidogo kichwa kikiwa chini kidogo kuruhusu damu kushuka katika ubongo
  • Akiwa katika hali nafuu apelekwe hospitali haraka ambako atapewa matibabu ikiwa ni pamoja na kuongezewa maji au damu na kupewa dawa.
  • Ikiwa mgonjwa amepata mshituko kwasababu ya kuvuja damu nyingi, inapasa kwanza kuzuwia damu kuvuja kisha huduma zingine zifuate ikiwa ni pamoja na kumuwahisha hospitali




Jumatatu, 3 Aprili 2017

Madhara ya utando mgumu katika meno

Jua madhara ya utando mgumu kwenye meno (calculus)


     Utando mgumu kwenye meno kwa jina la kitaalamu huitwa calculus,  utando huu huwa mgumu kiasi kwamba hauwezi kutoka kirahisi. Huwa na rangi tofauti tofauti kuanzia njano hadi nyeusi kutokana na hatua ya ukuaji wake.



     Calculus hutokea baada ya mabaki ya chakula yenye bacteria kwa wingi kukaa kwa muda ndefu hadi miezi kadhaa.

Madhara ya calculus 


1. Memo kuoza


     Utando huu huweka makazi mazuri kwa bacteria ambao hupelekea meno kuoza. Pia huweza kupelekea mabaki ya chakula kuongezeka na kuwawezesha hawa bacteria kujipatia chakula na makazi mazuri. Shughuli za bacteria hawa hupelekea jino kuoza katika eneo hilo.

      Kuoza meno kunaathari kubwa kiafya kwani kunaweza kupelekea kupoteza meno na magonjwa makubwa hata kupoteza maisha.

2. Fizi kushuka chini na kuacha mzizi wa jino wazi


   Calculus hupelekea fizi kushuka chini na kuacha mzizi wa jino wazi,  hii inaweza kupelekea kuhisi ganzi au maumivu ya jino kutokana na mzizi kuachwa wazi. Pia inaweza kupelekea jino kulegea na kufikia hata ya kung'olewa.


  3. Magonjwa ya fizi


     Calculus inaweza kupelekea magonjwa ya fizi kama gingivitis na periodontitis.   Gingivitis ni ugonjwa ambao hupelekea fizi kuvimba na kutokwa damu zinapo guswa kidogo.

     Periodontitis ni magonjwa ya fizi na mifupa ya taya, huambatana na fizi kuvuja damu, kuvimba,  kuoza na kutoa usaha. Pia hupeleke kulika kwa mfupa wa taya na kufanya meno kulegea.


4. Kusababisha magonjwa ya moyo


     Maambukizi ya bacteria huweza kupenya na kuingia katika mfumo wa mzunguko wa damu. Hii huweza kusababisha magonjwa ya moyo na dumu katika damu.
Namna ya kuzuwia calculus

     Ili kuzuwia utando huu,  hakikisha unapiga mswaki wako vizuri namna inayoruhusu pande zote za meno zinakuwa safi. Jifunze namna ya kupiga mswaki ili kuhakikisha usalama wa kinywa chako.


     Tembelea hospitali katika kliniki ya kinywa na meno ili utando huu uondolewe.   Ikiwa utando huu umeleta madhara katika afya yako, hakikisha utando huu unatolewa na matibabu yanatolewa ili kuzuwia ukuaji na madhara tatizo yanayoweza kujitokeza.
 

Kwamawasiliano piga; 
+255752674467
+255676674467

Alhamisi, 30 Machi 2017

Jua sababu zinazozuwia mwanamke kushika ujauzito

Unazijua sababu zinazopelekea mimba kushindwa kutunga?

     Wapo watu wanao dumu katika ndoa zao kwa miaka mingi bila kupata mtoto. Watu wingi huwa wepesi kuwatupia wake zao lawama kwakudhani kuwa wao tu ndo chanzo.

   Hapa tutaangalia sababu zinazoweza kupelekea mwanamke kushindwa kushika ujauzito zinazosababishwa na mwanamke na mwanaume kama ifuatavyo;

1. Uzito

     Mwanamke mwenye uzito mkubwa 15% zaidi ya anavopasa kuwa nao huweza kupunguza uwezekano wa yeye kushika ujauzito.

     Pia alie na uzito mdogo 15% ya anavopasa kuwa inaweza kupunguza uwezekano wa kushika ujauzito.

2. Kubadilika kwa mpangilio sahihi wa homoni kwa mwanamke


     Kubadilika kwa mpangilio huo husababisha kuwa na mzunguko wa hedhi ndefu au fupi na huweza badilika badilika.  Kutokana na hilo mwezi mpevu huathiliwa.

3. Matumizi ya madawa


     Matumizi ya dawa za maumivu na za magonjwa ya muda ndefu inaweza kuzuwia mwanamke kushika ujauzito kwa kipindi fulani.

4. Matumizi ya tumbaku na pombe


      Matumizi ya vitu hivo vinaweza kupunguza uwezekano wa mwanamke kupata mimba.   Pia inaweza kusababisha mwanaume kusindwa kusababisha ujauzito kwa mwanamke.

5. Magonjwa ya mirija ya folopi na mji wa mimba.


     Magonjwa haya husababisha makovu katika mji wa mimba na na kufanya yai lililorutubishwa kutoweza kutungwa.

   Pia huweza kusababisha kuziba kwa mirija hiyo na kupelekea kuzuwia urutubishaji.
  Maranyingi magonjwa haya huwa ya zinaa ingawa kansa ya uzazi na ovari husababisha utasa pia.

6. Mwanaume wenye historia ya magonjwa kama tezi dume na maambukizi katika via vya uzazi pia yanaweza kupunguza uwezekano wa kusababisha mimba.
Add caption

Jumatatu, 27 Februari 2017

Ongeza uwezo wa ubongo wako kwa kufanya haya

Jifunze namna ya kuongeza uwezo wa akili yako


     Watu wingi huamini kuwa uwezo wa ubongo hupungua mtu anavo kuwa, lakini ubongo wa binadam huweza kuendelea na kazi yake vizuri tu hadi uzeeni endapo ubongo utakuwa na hali nzuri kiafya. Kwani seli za ubongo huweza kuzalishwa ikiwa utakuwa na afya njema.

     Ili kuongeza uwezo wa ubongo wako yapo mambo muhimu ya kuzingatia. Mambo haya yatasaidia ubongo wako kuwa imara kwani uwezo wa kufanya kazi kama uwezo wa kufikiri na kutunza kumbukumbu utaongezeka.

     Yafuatayo yatasaisia ubongo wako kufanya kazi kwa ufanisi zaidi hadi katika hali ya uzee.


1. Kucheka na kufurahi


      Moja kati ya vitu muhimu ili kufanya afya ya akili kuwa safi ni kupata nafasi ya kucheka na kufurahi. Kucheka hufanya kuzalishwa kwa seli za akili ambazo hufanya ubongo kuendelea kudumu kuwa na ngufu hadi uzeeni.

     Nivema kutafuta fulsa mbalimbali zitakazo kiwezesha kucheka na kufurahi katika mazingira mbalimbali ya maisha yako.

2. Kuvuta pumzi ndefu


     Kuvuta pumzi ndefu husaidia kupandisha dumu juu ikiwemo katika ubongo, pia husaidia kupunguza uwoga pale unapotarajia kufanya jambo.

     Nivema kwa siku baadhi kuwa unapata nafasi ya kuenda sehemu tulivu pekeyako na kukaa kisha unavuta pumzi ndefu na kushusha. Zoezi hili unaweza kulifanya ndani ya dakika 5 dadi 10.

     Baada ya hapo unaweza kuendelea kutulia na unaweza kufumba macho ukisikia sauti za ndege, au maji yanayo tembea au sauti za magari huku ukitafakari.

     Pia unaweza kuvuta pumzi ndefu kabla ya kuanza mtihani wako ili kupandisha damu juu na kupunguza woga wa mtihani.

3. Kushiriki mambo mbalimbali ya kijamii


     Inatakiwa mtu asiwe wa kukaa pekeyake bila kushiriki mambo ya kijamii kama yakidini, misiba au kubdilishana mawazo mbalimbali.

     Kushiriki mambo ya kijamii huimarisha akili na kufanya kuwa yenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi pale inapo hitajika. Hii huambatana na kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo za pamoja.

4. Kuchangamsha na kuburudisha akili akili


      Kunawakati akili huhitajika kuburudishwa na kuchangamshwa kwa kufanya mambo kama vile kutalii mbuga za wanyama, kutoka na familia kujivinjari, kuangalia michezo ya video, kucheza wimbo au kucheza gemu.

     Kuchangamsha akili huifanya akili yako iweze kujijenga vizuri zaidi.

5. Kuipatia akili changamoto


      Ili kuongea uzalishaji wa seli za ubongo na kuifanya akili yako kuwa imara na uwezo wa kutunza kumbukumbu, akili inahitajika kupewa changamoto na sio kuishi bila kufanya akili kuweza kujishughilisha. Changamoto hizo ni kama kujifunza kitu kipya kama lugha, kupiga kinanda au gitaa au kupata habari mbalimbali za ulimwengu.

6. Kulala


     Kulala ni muhimu kwani hupumzisha akili yako, ikiwa umelala na mambo kichwani huyapanga vizuri ili kufa yawekwe katika kumbukumbu nzuri. Pia huweza kuuandaa ubongo vizuri kwaajiri ya kupokea mambo mapya.

      Nivizuri kwa mtu mzima kulala kati ya masaa 7.5 ha 8.5, na nivizuri zaidi ikawa utalala usingizi wa usiku usio na ghasia za kushituliwa kutoka usingizini.

7. Kurudiarudia jambo na kulihusianiasha na uhalisia


     Kurudiarudia jambo huweza kufanya kumbukumbu yake isipotee kwa wepesi. Na nivema zaidi jambo jipya kurudiwa tena siku hiyohiyo ili kuliingiza katika kumbukumbu ya muda mrefu.

     Pia jambo geni linaweza kuhusianishwa na linalofahamika ili kufanya jambo jipya kudumu akilini. Mfano unaweza kuandika kifupi cha maneno ya kile unachojifunza, nakifupi hicho kinakuwa na maana fulani inayo fahamika.


8. Mazoezi ya viungo


     Mazoezi ya viungo husaidia akili kuwa imara kwa husaidia kuongezeka kwa uzalishaji wa seli za ubongo. Pia mazoezi huasaidia kupandisha damu kwenye ubongo na kuufanya kupata chakula na oksijeni ya kutosha. Ubongo hutumia 20% ya oksijeni yote ya mwilini hivyo ongezeko lake kuongeza ufanisi wa ubongo.

     Mazoezi husaidia kupunguza uwezekano wa magonjwa ya mishipa ya damu na moyo na kisukari, kutokana na magonjwa hayo kuhafifisha ufanisi wa utendaji wa ubongo, kuyazuwia huweza kuongeza nguvu ya ubongo na akili.


9. Kupata chakula kinachoimarisha ubongo


   Chakula chenye wingi wa omega-3-fati kama vile samaki, ini, ubongo na vinginevyo husaidia kimarisha ubongo. Kutokana na mwili kutokuwa na uwezo wa kuzalisha vyakula hivo, inahitajika kula kutoka kwa vyanzo vingine kama samaki.

   Ili kuboresha ufanisi wa kazi ya ubongo na akili, fanya mambo hayo kama yanavo jieleza.

Endelea kufuatana nami katika mambo mbalimbali ya afya kupitia blog yangu au piga simu;
0752674467
0676674467
 

Jumanne, 21 Februari 2017

Namna ya kumpata mtoto wa kiume au wa kike

Jua namna ya kumpata mtoto wa kiume au wa kike


   Watu wingi wamekuwa wakitamani kupata mtoto wa jinsia fulani kutokana na kupata watoto wa jinsia moja tu. Wengine hutamani mara tu baada ya kuingia katika ndoa wapate mtoto wa jinsia wanayoipenda.

  Iko wazi kuwa kuzaa mtoto wa jinsia fulani ni mpango wa mwenyezi Mungu, lakini mwanadamu amepewa sehemu kidogo sana ya kukamilisha uumbaji. Kwasababu hiyo kukawa na wanasayansi ambao hufunuliwa vitu vichache ili kila mwenye kutaka kujifunza aweze kukamilisha uumbaji wake. Hivo wewe pia unanafasi ya kufanya kitu kwa sehemu fulani kikawa na hujachela.

   Iko wazi kuwa mtu anaweza kupanga na mwenzi wake wazae mtoto wa jinsia gani kwa wakati gani. Kwakuwa sisi wanadamu sio waumbaji, hili huwa ni kwa uwezekano (probability) na ukiwa makini kabisa kunakuwa na uwezekano mkubwa sana wa kupata kile ulicho hitaji kuliko vinginevyo.


   Ili kujua namna ya kupata mtoto wa jinsia fulani, unatakiwa kwanza kujua niwakati gani unaweza kupata mtoto.

   Soma kwa makini mchoro hapo chini kisha ufuatane nami katika maelezo yanayo fuata.

   Wakati wa kushika ujauzito


   Mzunguko wa hedhi ya mwanamke iliyo sawia hukamilika kwa siku 28. Kwa kawaida wanawake wengi huwa na hedhi yenye mzunguko wa siku 28 hadi 32, ingawa wapo wengine huwa na mzunguko mfupi wa siku 14 hadi 25 na wengine mrefu zaidi hadi kufikia siku 42.

   Hapa tutaongelea mtu mwenye mzunguko wa siku 28.

   Siku ya kwanza huanza kuhesabiwa pale tu mwanamke anapoingia hedhi, kama ameingia tarehe 8 basi tarehe hiyo itakuwa siku ya kwanza ya mzunguko wake, na mzunguko wake utaisha pale atapoingia hedhi inayofuata.

   Mfano, akiingia tarehe 8 mwezi wa tano na kuingia tena tarehe 6 mwezi wa sita, basi mzunguko wake utakuwa una siku 29. Kumbuka siku ya kwanza kuingia hedhi ya mwezi unaofuata haihesabiwi katika mzunguko ulionao kwa wakati huo, huhesabiwa kama siku ya kwanza ya mzunguko unaofuata.

   Mwanamke anaweza kuingia hedhi na siku ya tano akatoka, siku ya Kumi na moja ndipo uwezekano wa kushika mimba huanza kuwa. Hii ni kutokana na kukomaa kwa yai lake na kuwa pevu na hutalajia kutoka katika ovari.

   Wastani wa siku anayoingia katika mwezi mpevu (ovulation) ni siku ya 14. Yai hili huweza kukaa masaa 12 hadi 24, baada ya hapo hufunga na kuto kuruhusu urutubishaji.

  Mbegu za mwanaume huweza kukaa hadi siku tatu tangu kuingia katika via vya uzazi vya mwanamke, baada ya hapo huharibika. Kutokana na hilo mwanamke anae tarajia kuingia mwezi mpevu siku ya 13 au 14 akikutana na mwanaume siku ya 11 au 12 anaweza kushika mimba.

   Mwanamke aliyeingia mwezi mpevu siku ya 14 au 15 akikutana na mwanaume siku ya 15 au 16 anaweza kushika mimba.

   Mwanamke akikutana na mwanaume siku ya 14 huwa na uwezekano mkubwa sana wa kushika mimba. Uwezekano wa kushika mimba huongezeka kutoka siku ya 11 hadi 14, na huanza kupungua tena kutoka siku hiyo hadi ya 16.

   Uwezekano wa kushika mimba siku ya 1 hadi ya 10 huwa mdogo mno, kuanzia siku ya 17 hadi 28 pia uwezekano huwa mdogo mno. Mimba inapotokea katika vipindi hivo huwa kuna sababu nyingine zinazo pelekea.


Namna ya kumpata mtoto wa kike


   Anza rasmi kukutana na mpenzi wako siku ya 11 na 12. Katika siku ya 11 anza kuweka mbegu hata mara moja tu au mara mbili, ui pizi maranyingi sana acha nafasi ukutane nae siku ya 12.

   Baada ya hapo mwache ili akiingia mwezi mpevu, yai lake likutane na mbegu zilizo himili kuendelea kuwepo ambazo huwa x, hizo huishi muda mrufu na kuvumilia hali na ndizo husababisha mtoto wa kike.

Namna ya kumpata mtoto wa kiume


   Nivema kukutana usiku wa kuamkia siku ya 14 na siku ya 14 yenyewe. Pia ukikutana nae siku ya 15 au 16 ikawa yai lake bado halijafunga, unaweza kupata mtoto wa kiume.

   Hii ni kutokana na mbegu za kiume kuwa na wepesi wa kuenda na kukutana na yai lililo tayari pevu. Yai linapokuwa tayari mbegu y huwa na uwezekano mkubwa sana wa kurutubisha yai hilo na kusabisha mtoto wa kiume.

   Kutokana na mbegu hizi kutokuwa na ustahimilivu wa hali, hakikisha unakutana na mwanamke ambaye yuko vizuri kisaikolijia, anaefurahia tendo la ndoa. Upatikane muda mrefu wa kumuandaa ili azalishe ute mwingi utakao saidia mbegu kusafiri kwa wepesi na usalama mpaka katika mirija ya folopia ambako urututushaji hufanyikia.

   Sio mbegu zote zinazoweza kufika katika eneo la urutubishaji nyingi hufia nyiani, ni chache na nyingi huwa za kikehasa pale mazingira yapokuwa si mazuri. Za kiume huwa hodari zaidi mazingira yanapo kuwa mazuri ingawa maisha yake huwa mafupi.

NB: Uwezekano wa kupata mtoto wa kiume au wa kike huwa kwa mwanaume, yeye ndo anaweza sababisha mabadiliko yoyote ingawa mwanamke mwenye ushirikiano mzuri kwa mwanaume humwongezea mwanaume uwezekano wa kumpata mtoto anaemtaka.


Endelea kufuatana nami, au piga simu
0752674467
0676674467
 ibrahimmamboleo09@gmail.com

Jumapili, 19 Februari 2017

sababu zinazo pelekea kushindwa kushika ujauzito

Sababu zinazo weza kuzuwia mimba kutunga




   Watu wengi hudhani kuwa niwakati tu umri umeenda ndo sababu ya mwanamke kushindwa kushika mimba. Nawengine hulaumu wanawake kwanini hawazai bila kujua sababu zinazo weza pelekea hali hiyo.

 Zipo sababu zinazoweza kupelekea mwanamke asishike mimba, nyingine zikiwa zinachangiwa na mwanaume na nyingine mwanamke mwenyewe.

Sababu zinazoweza kupelekea hali hii

1. Mtindo wa maisha

     Ipo mitindo ya maisha ambayo hushusha afya ya mtu kama vile uvutaji sigara, matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye caffeine kwa wingi, bangi, ulevi na utumiaji wa madawa mengine ya kulevya.

      Hii hupelekea kupunguza uwezekano wa kutunga mimba na inamuathiri mtu wa jinsia yoyote.

     Maisha haya yanaweza kupelekea uzalishaji wa mbegu zisizo komaa au mbegu kidogo  za kiume na kupunguza uwezekano wa urutubishaji.
2. Magonjwa ya zinaa

     Magonjwa ya zinaa yaliyomengi huwa hayaoneshi dalili kwa wanawake hivo yanapo kuwa hayajatibiwa huweka makovu katika mji wa mimba.

     Hili hupelekea mimba kutotungwa hatakama urutubishaji wa yai la mwanamke umeshafanyika.

     Pia magonjwa ya zina yanaweza kuathiri mirija ya mwanaume ya kupitisha mbegu ikapelekea asitoe mbengu wakati wa tendo la ndoa.

3. Magonjwa ya mji wa mimba na mirija ya folopia

    Majonjwa yanayo athiri mirija ya folopia kama Kansa na baadhi ya magonjwa ya zinaa, yanaweza kupelekea kuziba kwa mirija hiyo. Hili huzuwia mbegu za kiume kukutana na yai ili kurutubisha.

    Pia magonjwa haya huweza kusababisha makovu na kuongezeka kwa ukuta wa mji wa mimba, kutokana na hili mimba inashindwa kutungwa.

    Wakati mwingine Kansa inaweza kuathiri ovari ambazo ndizo huhusika na uzalishaji wa mayai ya kike.

4. Homoni kushindwa kuwa na uwiano sawa

    Kutokuwa na mpangilio unaoeleweka wa majira ya mzunguko wa hedhi kwa mwanamke hutokana na kutokuwa na mpangilio sahihi wa homoni. Hii inaweza kufanya wakati halisi wa kushika mimba usijulikane na kupelekea mimba kutotungwa kwa wakati wapenzi wanapo hitaji mtoto.

5. Unene
    Mwanamke akiwa na uzito na unene mkubwa anaweza sababisha kutotungwa kwa mimba kutokana uwezekano wa kuzalisha kiwango kikubwa cha homoni oestrojeni inayozuwia mimba kutungwa.

6. Umri

     Mwanamke anapofikia umri wa miaka 43, uwezekano wa yeye kushika mimba huwa mdogo. Kwakadri umri wa mwanamke unavyoongezeka na idadi na ubora wa mayai yake hupungua pia.

7. Chakula

    Mwanamke anaekosa afya nzuri kutokana na upungufu wa virutubisho mwilini hupunguza uwezekano wa kushika mimba.

8. Madawa

    Badhi ya madawa kama yanayotumika kipunguza maumivu na kutibu magonjwa sugu kama kansa yanaweza kusababisha kupungua kwa uwezekano wa mwanamke kushika mimba.

9. Kutoelewa wakati wa kushika mimba

    Baadhi ya watu hushindwa kujua wakati sahihi wa mwanamke kushika mimba. Hii hupelekea wapenzi kukutana wakati ambao sio muafaka na kufanya wakakaa muda mrefu bila kupata mtoto.
 
   Wapenzi wanaweza kishi kwa miaka kadhaa kisha wakapata mtoto au wanaweza kuza mwanzo kisha hali ya kutoshika mimba ikajitokeza, moja kati ya sababu hizo inaweza sababiash na sio ajabu.

   Inahita kukaa chini mwanake na mwanaume kuona tatizo linaweza kuwa nini, na sio kumwachia mwanmake pekeyake.



Endelea kufuatana nami katika maada mbalimbali au piga simu:
0752674467
0676674467

Vyakula kwaajiri ya afya ya ngozi


Jua vyakula 10 kwa afya ya ngozi yako


      Afya ya ngozi ni jambo ambalo kilamtu anahitajika uitunza na kuiimarisha ili kujikinga dhidi ya magonjwa ya ngozi na kuongeza mvuto wa ngozi yake kwa watu. Watu wengi wamekuwa wakitafuta vipodozi mbalimbali ili kujichubua ngozi zao jambo ambalo huhatarisha afya ya ngozi zao na kupelekea magonjwa mbali mbali ya ngozi ikiwamo kansa ya ngozi.

     Fuatana nami ili kujua namna ya kuifanya ngozi yako kuwa yenye afya, mvuto na rangi yake asili.

     Vipo vyakula Vingi ambavyo vikitumiwa vizuri hufanya ngozi yako kuwa bora zaidi, hapa tutajadili vyakula Kumi muhimu ili kuimarisha ngozi yako.

1. Viazi vitamu
   Viazi vitamu vina wingi wa vitamini A ambayo hupunguza ngozi kukunjamana na kuondoa dalili za uzee.

2. Parachichi
   Tunda hili lina wingi wa viamini A na C na nyuzinyuzi, virutubisho hivi husaidia kuzuwia mikunjamano ya ngozi, ngozi kuzeeka mapema, kukinga dhidi ya maradhi na nyuzinyuzi husaidia mmeng'enyo wa virutubisho hivo.

3. Vyakula vya ngano
   Vyakula vya ngano kama mkate, chapati au ngano iliyo chemshwa hulinda,  kuimarisha ngozi nakuifanya kuwa laini. Inashauliwa kutumia vyakula vya ngano ya kahawia na sio nyeupe ili kuimalisha mmeng'enyo wa chakula na afya yako.

4. Samaki
   Katika samaki kuna wingi wa protini na vitamini B12 muhimu kumarisha ngozi yako na kuifanya laini na yenye mvuto.

5. Chungwa
   Chungwa ni tunda muhimu kwa ngozi yako kwani huilinda ngozi dhidi ya mionzi ya jua ambayo huathiri ngozi. Utafiti uliofanyika na chuo cha Arizona ulionesha kuwa 33% ya watu waliotumia sana machungwa walijilinda dhidi ya mionzi ya jua inayoathiri ngozi.

6. Karoti
   Karoti huimarisha ngozi na kifanya iwe na mvuto zaidi kutokana na kuwa na wingi wa carotenoid ambayo huimarisha ngozi na kuifanya iwe na afya nzuri na ranging inayovutia.

7. Chokoleti (chocolate)
   Chokoleti huisaidia ngozi kuwa yenye unyevu na laini, hii huifanya ngozi iwe kama imepakwa kipodozi kwani huwa na mng'o wenye mvuto.

8. Boga
   Maboga huwa na wingi wa beta-carotine ambayo hubadilishwa na kuwa vitamini A ambayo hufanya ngozi yako kuwa yenye afya na isiyo na mikunjo.

9. Mayai na maini
    Vyakula hivi huwa na wingi wa vitamini B na protini ambayo hutengenezwa kuwa seli za ngozi zinazokufa ili kuimarisha na kuboresha ngozi yako.

10. Maji
     Maji huwa na molekyuli (molecules) ambazo husaidia shughuli za kiseli na huunganika katika seli za ngozi kuifanya laini na yenye mwonekano wa ngozi yenye afya. Ngozi iliyopungukiwa maji kupauka na kukosa mvuto. Hii huonekana zaidi mtu anapoishiwa maji mwilini na ngozi yake hupauka.




   Usipende kutumia vipodozi vyenye kemikali kali ikiwemo mekyuri kwani utaharibu ngozi na kusababisha kansa ya ngozi kutokana na kemikali hizo. Na pia vipodozi hivyo vinaweza kuruhusu mionzi ya jua kuathiri ngozi yako.

     Nivema kutumia vipododozi visivyo na kemikali kali huku ukuendelea kujipatia vyakula kama hivyo tulivyo viangalia. Hii itafanya ngozi yako kuwa nzuri zaidi na yenye afya.
Fuatana nami katika maada mbalimbali katika blog yangu au piga simu:
0752674467
0676674467

Jumamosi, 18 Februari 2017

Unajua namna ya kuzuwia meno kuoza?

Zuwia meno kuoza


      Kuoza meno ni ugonjwa wa meno unaosababishwa na asidi inayozalishwa na bacteria wanaoishi mdomoni( normal flora). Asidi hii huondoa madini kama calcium ambayo huimarisha meno na mifupa.

     Ili bacteria waweze kusababisha uzalishaji wa asidi kwa wingi inayoweza kupelekea meno kuoza, kinahitajika chakula cha sukari ambacho ndicho hubadilishwa na bacteria hao kuwa asidi inayopelekea meno kuoza.

     Sio kila chakula cha sukali hupelekea meno kuoza, isipokua vyakula vya sukari vinavyo zalishwa viwandani (cariogenic foods) kama vile soda, pipi, chokleti, sukari nk.

     Vyakula vya asili na vyenye sukari kama vile viazi vitam, ndizi mbivu, nanasi, muwa nk, haviwezi kusababisha meno kuoza.

    Kwakadiri miaka inavoendelea na utandawazi kuongezeka ndivyo watu wanaachana na vyakula asili, hili hutoa jibu kwanini miaka ya sasa tatizo hili linaongezeka ukilinganisha na zamani.


 Mambo yanayo pelekea meno kuoza

 1. Sukari

Matumizi ya sukari Mara kwa mara husababisha uzarishwaji wa asidi kwa wingi inayopelekea meno kuoza.

Hoja sio uwingi wa sukari ila idadi ya matumizi kwa siku (frequency). Je, vyakula hivi hutumiwa marangapi kwa siku? ongezeko la matumizi huhatarisha meno kuoza hatakama unapiga mswaki.

2. Bacteria

     Aina ya bacteria waliopo mdomoni na ukuaji wake (ongezeko lake) hupelekea ongezeko la uzalishaji wa asidi hatari kwa meno.

      Bacteria huongezeka zaidi pale kinywa kinapo kuwa kichafu chenye mabaki mengi ya chakula ya muda mrefu ambayo hubadilishwa  na kuwa ugaga(vitu vigumu vilivyo ganda juu ya meno). Vitu hivi hutengeneza makazi mazuri ya bacteria.


3. Meno yenyewe

     Kuoza kwa meno hutegemeana na hali ya mwili ya mtu binafi kuweza kupambana dhidi ya tatizo. Hivyo wapo watu ambao kinga ya meno yao dhidi ya kuoza ni kubwa zaidi ya wengine.

4. Muda

     Meno huchukua muda mrefu mpaka kufikia yanaoza ukayagundua, sio jambo la siku chache bali ni la miezi kadhaa hadi miaka.


Matokeo ya baadae ya kuoza meno

   Jino kuuma au kuhisi ganzi linapopitiwa na vitu vya baridi na moto au vyenye sukari.
kupoteza jino, jino kung'olewa endapo limelika sana au pale linaposababisha magonjwa mengine mdomoni.

    Majipu ya mdomoni yanaweza kusababishwa na meno kuoza hasa pale bacteria wanapo pata nafasi ya maambukizi.
    Maambukizi ya  mfupa wa taya (ostemylitis), hili linaweza kupelekea kukatwa sehemu au kuondoa taya lote.

    Kifo, mtu akipata magonjwa kama majipu makubwa, Kansa au maambukiza katika misuli ya usoni, anaweza kupoteza maisha.

Namna ya kuzuwia

     Ili kuzuwia meno kuoza inapasa kupunguza utumiaji wa sukari mara kwa mara, utumiaji usizidi mara tatu kwa siku.

      Piga mswaki walau mara mbili kwa siku, asubuhi na jioni kabla ya kulala yaani baada ya chakula cha usiku. Jifunze namna ya kupiga mswaki kwa usahihi ili kuhakikisha kinywa chote kinawekwa safi.

     Sukutua kinywa chako kila baada ya kutumia vyakula vya sukali vizalishwavyo viwandani kama vile pipi.

     Epuka kulala usingizi na vyajula hivi mdomoni, hakikisha pia mtoto halali na vyakula hivi mdomoni.

     Tembelea mara kwa mara kliniki ya meno walau mara mbili kwa mwaka ili kuchunguza kama kunadalili ya kuoza meno. Hili itakusaidia kujua na kukinga matatizo mengine ya kinywa na mano.

    Tumia dawa ya meno wakati wa kupiga mswaki, hakikisha dawa unayotumiwa ina fluoride. Flouride husaidia kurudisha madini katika meno.

     Nenda kliniki ya meno endapo una meno yaliyooza ili uyazibe kwa dawa yasindelee kuoza. Watu wengi kuenda kliniki baada ya maumivu jambo ambalo hupelekea jino kung'olewa.


Usikubali kupoteza jino lako hata moja kwani linakazi yake muhimu.



Fuatana nami katika blog yangu au piga simu:
+255752674467
+255676674467

 
Maada zinazo fanana
Afya ya uzazi na mahusiano
Afya ya mama na matoto
Afya ya mwili na akili nk

Ijumaa, 10 Februari 2017

kutokwa harufu mbaya ukeni

Sababu za kutokwa harufu mbaya ukeni



    Tatazo hili limekuwa likiwakabili baadhi ya wawake na wengi  wao wamekuwa wakitafuta suruhisho lakini wakakosa.

    Kutokwa harufu ukeni ni jambo ambalo linaweza kupunguza nguvu ya upendo katika mahusiano ya kimapenzi ya wana ndoa. Kwakuwa harufu inaweza sikika zaidi wakati na baada ya tendo la ndoa, mwanaume anaweza kushindwa kuivumilia na kutokuwa na hamasa ya kufanya tendo hilo.

   Baadhi ya wanawake wamekuwa wakidhani harufu haipasi kutoka katika uke hilo sio sahihi, isipokua kama sehemu nyingine za viungo uke pia unatoa harufu ambayo ni yakawaida isiyo ambatana na dalili zozote za kuashiria ugonjwa.

    Harufu kidogo inaweza kutoka hasa baada ya kutoka hedhi na baada ya tendo la ndoa pale mbegu za kiume zinapo kutana na uke na kubadili hali ya asidi-basi yake, na hili linaweza kuwa la kawaida na hutokea kutegemeana na mwanamke.

   Tatizo huwa pale ambapo harufu inakuwa kali zaidi au pale harufu inapoendelea kwa siku nyingi baada ya kutoka hedhi, hili huashiria maambukizi ya ugonjwa au sababu nyingine tutakazo ziangalia.

   Tutangalia sababu ya tatizo hili na namna ya kutibu.
 
   Sababu zinazo pelekea tatizo

1.  Kutokuwa msafi wa mwili
   Kama ilivyo kawaida kwa ngozi kutoa harufu pale jasho linapo mtoka mtu, pia mtu asiye msafi hasa katika sekemu za nje za uke anaweza kutoa harufu mbaya, na husikika hasa wakati wa tendo la ndoa na baada ya kazi.

    Hili ni kutokana na kuwepo kwa tezi zinazotoa kemikali kama vile zitoavyo za sehemu nyingine kama kwapa.

2. Maambukizi
    Harufu inapokuwa mbaya na kali na wakati mwingine kama harufu ya samaki, huwa ni kwasababu ya maambukizi.

    Harufu huambatana na muwasho au maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa na wakati wa kukojoa.

    Yapo magonjwa ya sehemu za uke yanayo sababisha harufu na yanasababishwa na baadhi ya protozoa, fangasi na bacteria.

3. Mabadiliko ya homoni mwilini

   Katika nyakati mbalimbali ndani ya mzunguko wa hedhi, hutokea mabadiliko aina mbalimbali ya homoni. Wakati ambao harufu inaweza kuongezaks ni ule ambao homono aina ya oestrogeni inapokuwa imepungua mwilini mwa mwanamke hasa zile siku zinazokamilisha mzunguko wa hedhi. Wastani wasiku Kumi kabla ya kuingia hedhi.

4. Chakula unachokula

   Vipo aina ya vyakula ambavyo huwa na harufu kali kama vitunguu swaumu, samaki, kabeji nk. Utafiti unaonesha kuwa vyakula hivi vinapotumiwa husababisha harufu ya ngozi na uke kuongezeka.

5. Kusaulika au kuachwa kwa pedi kwa muda mrefu
   Kuachwa kwa pedi muda mrefu kunaweza kusababisha ongezeko la ukuaji wa bacteria, jambo hili pia linaweza kuzalisha harufu mbaya.

6. Kutawadha uke kwa maji.

   Kusafisha sana uke mara kwa Mara huondoa aina ya bacteria wasio dhuru ambao huhakikisha wanailinda sehemu ya uke dhidi ya maambukizi na magonjwa.

   Inapasa kusafisha katika sehemu za nje za uke wakati wa kuoga pia baada ya haja ndogo ili kuweka sehemu hizo kuwa safi.

Namna ya kukinga

Ili kukinga tatizo hili, yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa:

    Kuhakikisha hali ya usafi wa mwili na sehemu za siri.

   Badili nguo hasa za ndani baada ya mazoezi au kazi.

   Vaa nguo za ndani nyepesi, zisizo bana na za matilio ya pamba (cotton).
    Usijitawadhe ndani ya uke.
  Punguza unene na uzito endapo unahisi ni chanzo cha kutoa jasho mara kwa Mara.

Tiba ya tatizo

    Ikiwa unatokwa usaha, unahisi muwasho na harufu mbaya ukeni, nenda hospitality au kituo cha afya kilicho kari nawe umwone daktari hili afanye uchunguzi madhubu na kukupatia matibabu. Matibabu yapo kutegemeana na aina ya vimelea walisababisha ugonjwa huo.

   Hizi dalili huja endapo umepata maambukizi, na maambukizi hayo hupona haraka yakiwahiwa kwa matibabu.

Endelea kufuatana nami katika maada za afya katika makala zangu katika blog yangu, au piga simu :
+255752674467 au
+255676674467

Maada zinazo fanana
Afya ya mama na mtoto
Aya ya kinywa na meno
Afya ya mwili na akili nk

kutokwa harufu mbaya mdomoni

Je, unazijua sababu za kutokwa harufu mbaya mdomoni?




   Tatizo hili linawakabili watu wengi, katika jamii ya kitanzania, kati ya watu wanne basi mmoja anaweza kuwa anakabiliana na tatizo hili japo kwa kiwango tofauti.
 
   Wapo wanaojigundua kuwa wanatatizo na wengine hawajigundui mpaka atapoambiwa na jirani yake ama mpenzi wake. Maranyingi watu hushindwa kuwaambia wenzao endapo wamegundua kuwa mwenzao anatatizo hilo kwani ni la aibu hivo kushindwa kujitambua.

   Wengine hawagunduliki kutokana na tatizo kuwa dogo kwao yani harufu kuwa kidogo sana mpaka pale tu anaposogelewa zaidi na mwenzake.

   Urafiki au mapenzi ya watu yanaweza kuvunjiki ikiwa mmojawapo akiwa na tatizo hilo, hivo fuatana nami ujue kwanini tatizo hilo linatokea, namna ya kuzuwia na kutibu.

Sababu zinazoweza kupelekea tatizo hili
    Zipo sababu kadhaa zinazo weza kusababisha tatizo la kutoa harufu mdomoni, hapa tutaangalia chache tu ambazo zinaweza kukusaidia kwa sehem kubwa.

1. Kuto kuweka kinywa (mdomo) katika hali ya usafi.
   Kinywa kisipo safishwa hubaki na mabaki ya chakula ambayo huvunjwavunjwa na bacteria na kuzalisha kemikali zinazo sababisha harufu mbaya. Bacteria huweza kuvunjavunja mabaki kwa kasi kutegemaeana na wingi wake na hali ya kinywa.

   Njia kuu za kuweka kinywa safi ni pamoja na kupiga mswaki na kuchokonoa meno kwa vijiti (sticks).

   Baadhi ya watu hawajui kupiga mswaki kwani hushindwa kufikia baadhi ya kuta za meno hasa magego ya mwisho hivo tatizo la harufu mbaya kuendelea.

   Kitaalam inashauliwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku, asubuhi kabla au baada ya chai na baada ya chakula cha jioni yaani kabla ya kulala. Ili kulinda meno zaidi nivema kutosukutua kwa maji baada ya kupiga mswaki.

2. Uvutaji wa sigara namatumizi ya mazao ya tumbaku kama vile kubeli na ugoro vinaweza kuwa sababu ya kutoka harufu kinywani.

3. Matumizi ya baadhi ya vyakula vinavyotoa harufu mbaya kama vitunguu swaumu na matumizi ya pombe. Nivema kupiga mswaki au kutafuna chakula chenye harufu nzuri kama bigijii na pipi baada ya kutumia vyakula kama vitunguu swaumu.

4. Magonjwa ya fizi na taya (periodontitis).
    Yapo magonjwa yanayoweza kusababisha kutoa harufu hasa kwa mtu mwenye ugonjwa wa kuozesha fizi (necrotizing gingivitis) au majipu ya fizi. Kutokana na shughuli za bacteria katika hizi fizi, harufu huzalishwa.

5. Magonjwa ya njia za hewa na mapafu pia huweza kusababisha harufu mbaya kutoka kinywani.

Namna ya kukinga
   Namna ya kukinga tatizo hili inategemeana na sababu iliyopelekea tatizo hili. Hizi hapa ni njia za kuzuwia na kuondoa tatizo hili:

   Kuhakikisha kinjwa kinakuwa safi kwa kupiga mswaki kila pande za kila jino na kupitisha mswaki juu ya ulimi. Unaweza kutumia wastani wa dakika 5 kuhakikisha umepiga mswaki vizuri.

   Tumia vijiti kuchokonoa meno ili kuondoa mabaki kati ya meno ambapo mswaki hauwezi kupita. Hilo linatakiwa kufanyika taratibu kuzuwia kujiumiza fizi.

   Kusukutua kwa aina ya dawa ya maji (antibacterial mouth rinse), hii inaweza kupatikana katika maduka ya madawa au hospitali na katika vituo vya afya.

   Tumia vyakula vyenye harufu nzuri baada ya kutumia vile vyenye harufu mbaya.

   Acha matumizi ya sigara na mazao yake kama kubeli.

   Nenda hospitaliti na umwone daktari wa kinywa na meno endapo unahisi kuwa harufu ya kinywa chako inatokana na magonjwa ya fizi au mingineyo.



Ili kufaham zaidi kuhusu afya ya kinywa na meno, endelea kufuatana nami katika makala mbali mbali au piga  simu:
+255752674467 au
+255676674467
JINA: Ibrahim Mamboleo

Maada zinazo fanana
>Afya ya mama ma mtoto
>Afa ya uzazi na mahusiano
Afya ya mwili na akili nk