Ugonjwa wa kuoza fizi
Ugonjwa wa kuoza fizi ni ugonjwa unaotokea Mara chache na hutokea zaidi katika nchi zinazoendelea Kama Tanzania hasa katika maeneo ya watu maskini. Ugonjwa huwa hatari ikiwa utaendelea sana na kusababisha fizi kuozasana has a pale unapopelekea maambukizi ya magonjwa mengine.
Mambo yanayoweza kupelekea ugonjwa huu
- Kinywa kichafu, uchafu wa kinywa hupelekea kukua kwa bacteria hatari wanaoweza kupelekea ugonjwa.
- Uvutaji sigara na matumizi ya ugoro na kubeli yanaweza kupelekea tatizo.
- Afya mgogoro, mtu mwenye afya mgogoro anaweza kupelekea bacteria walio kinywani wasio na madhara kupelekea madhara na kusababisha ugonjwa.
- Msongo wa mawazo
- Kinga ya mwili kushuka kutokana sababu mbalimbali ukiwemo UKIMWI au magonjwa sugu kama kisukari.
- Maambukizi ya magonjwa ya kinywa
Dalili za ugonjwa
Harufu mbaya ya kutoka kinywani na kuhisi radha mbaya
- Damu kuvuja katika fizi kwa urahisi
- Vidonda katika fizi
- Kuvimba fizi na kuwa njekundu
- Fizi kuuma
- Fizi koza na kupukutika
- Fizi kutokwa usaha
Matibabu
Unapoona dalili za namna hii hapo juu, nivema uende hospitality ili ukaonane na daktari wa kinywa na meno, ikiwa unashindwa kuhospitali, fanya yafuatayo- Safisha kinywa chako kwa maji na kitambaa safi na laini
- Nunua dawa ya kusukutua kinywani ( chlorhexidine ), sukutua kinywa chako kwa kufuata maelekezo utakayopewa unapoinunua.
- Tumia amoxicycilne na paracetamol endapo unahisi msumivu ya fizi au homa, unaweza kiongeza metronidazole (frajiri) endapo tatizo ni kubwa. Tumia dozi ya Sikh tank kwa hili dawa isipokuwa paracetamol ambayo unaweza kutumia kwa Siku 3, hakikisha unafuata maelekezo ya matumizi ya dawa hizo uliyopewa wakati unazinunua.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni