Jumapili, 19 Februari 2017

Vyakula kwaajiri ya afya ya ngozi


Jua vyakula 10 kwa afya ya ngozi yako


      Afya ya ngozi ni jambo ambalo kilamtu anahitajika uitunza na kuiimarisha ili kujikinga dhidi ya magonjwa ya ngozi na kuongeza mvuto wa ngozi yake kwa watu. Watu wengi wamekuwa wakitafuta vipodozi mbalimbali ili kujichubua ngozi zao jambo ambalo huhatarisha afya ya ngozi zao na kupelekea magonjwa mbali mbali ya ngozi ikiwamo kansa ya ngozi.

     Fuatana nami ili kujua namna ya kuifanya ngozi yako kuwa yenye afya, mvuto na rangi yake asili.

     Vipo vyakula Vingi ambavyo vikitumiwa vizuri hufanya ngozi yako kuwa bora zaidi, hapa tutajadili vyakula Kumi muhimu ili kuimarisha ngozi yako.

1. Viazi vitamu
   Viazi vitamu vina wingi wa vitamini A ambayo hupunguza ngozi kukunjamana na kuondoa dalili za uzee.

2. Parachichi
   Tunda hili lina wingi wa viamini A na C na nyuzinyuzi, virutubisho hivi husaidia kuzuwia mikunjamano ya ngozi, ngozi kuzeeka mapema, kukinga dhidi ya maradhi na nyuzinyuzi husaidia mmeng'enyo wa virutubisho hivo.

3. Vyakula vya ngano
   Vyakula vya ngano kama mkate, chapati au ngano iliyo chemshwa hulinda,  kuimarisha ngozi nakuifanya kuwa laini. Inashauliwa kutumia vyakula vya ngano ya kahawia na sio nyeupe ili kuimalisha mmeng'enyo wa chakula na afya yako.

4. Samaki
   Katika samaki kuna wingi wa protini na vitamini B12 muhimu kumarisha ngozi yako na kuifanya laini na yenye mvuto.

5. Chungwa
   Chungwa ni tunda muhimu kwa ngozi yako kwani huilinda ngozi dhidi ya mionzi ya jua ambayo huathiri ngozi. Utafiti uliofanyika na chuo cha Arizona ulionesha kuwa 33% ya watu waliotumia sana machungwa walijilinda dhidi ya mionzi ya jua inayoathiri ngozi.

6. Karoti
   Karoti huimarisha ngozi na kifanya iwe na mvuto zaidi kutokana na kuwa na wingi wa carotenoid ambayo huimarisha ngozi na kuifanya iwe na afya nzuri na ranging inayovutia.

7. Chokoleti (chocolate)
   Chokoleti huisaidia ngozi kuwa yenye unyevu na laini, hii huifanya ngozi iwe kama imepakwa kipodozi kwani huwa na mng'o wenye mvuto.

8. Boga
   Maboga huwa na wingi wa beta-carotine ambayo hubadilishwa na kuwa vitamini A ambayo hufanya ngozi yako kuwa yenye afya na isiyo na mikunjo.

9. Mayai na maini
    Vyakula hivi huwa na wingi wa vitamini B na protini ambayo hutengenezwa kuwa seli za ngozi zinazokufa ili kuimarisha na kuboresha ngozi yako.

10. Maji
     Maji huwa na molekyuli (molecules) ambazo husaidia shughuli za kiseli na huunganika katika seli za ngozi kuifanya laini na yenye mwonekano wa ngozi yenye afya. Ngozi iliyopungukiwa maji kupauka na kukosa mvuto. Hii huonekana zaidi mtu anapoishiwa maji mwilini na ngozi yake hupauka.




   Usipende kutumia vipodozi vyenye kemikali kali ikiwemo mekyuri kwani utaharibu ngozi na kusababisha kansa ya ngozi kutokana na kemikali hizo. Na pia vipodozi hivyo vinaweza kuruhusu mionzi ya jua kuathiri ngozi yako.

     Nivema kutumia vipododozi visivyo na kemikali kali huku ukuendelea kujipatia vyakula kama hivyo tulivyo viangalia. Hii itafanya ngozi yako kuwa nzuri zaidi na yenye afya.
Fuatana nami katika maada mbalimbali katika blog yangu au piga simu:
0752674467
0676674467

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni