Sababu zinazo weza kuzuwia mimba kutunga
Watu wengi hudhani kuwa niwakati tu umri umeenda ndo sababu ya mwanamke kushindwa kushika mimba. Nawengine hulaumu wanawake kwanini hawazai bila kujua sababu zinazo weza pelekea hali hiyo.
Zipo sababu zinazoweza kupelekea mwanamke asishike mimba, nyingine zikiwa zinachangiwa na mwanaume na nyingine mwanamke mwenyewe.
Sababu zinazoweza kupelekea hali hii
1. Mtindo wa maishaIpo mitindo ya maisha ambayo hushusha afya ya mtu kama vile uvutaji sigara, matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye caffeine kwa wingi, bangi, ulevi na utumiaji wa madawa mengine ya kulevya.
Hii hupelekea kupunguza uwezekano wa kutunga mimba na inamuathiri mtu wa jinsia yoyote.
Maisha haya yanaweza kupelekea uzalishaji wa mbegu zisizo komaa au mbegu kidogo za kiume na kupunguza uwezekano wa urutubishaji.
2. Magonjwa ya zinaa
Magonjwa ya zinaa yaliyomengi huwa hayaoneshi dalili kwa wanawake hivo yanapo kuwa hayajatibiwa huweka makovu katika mji wa mimba.
Hili hupelekea mimba kutotungwa hatakama urutubishaji wa yai la mwanamke umeshafanyika.
Pia magonjwa ya zina yanaweza kuathiri mirija ya mwanaume ya kupitisha mbegu ikapelekea asitoe mbengu wakati wa tendo la ndoa.
3. Magonjwa ya mji wa mimba na mirija ya folopia
Majonjwa yanayo athiri mirija ya folopia kama Kansa na baadhi ya magonjwa ya zinaa, yanaweza kupelekea kuziba kwa mirija hiyo. Hili huzuwia mbegu za kiume kukutana na yai ili kurutubisha.
Pia magonjwa haya huweza kusababisha makovu na kuongezeka kwa ukuta wa mji wa mimba, kutokana na hili mimba inashindwa kutungwa.
Wakati mwingine Kansa inaweza kuathiri ovari ambazo ndizo huhusika na uzalishaji wa mayai ya kike.
4. Homoni kushindwa kuwa na uwiano sawa
Kutokuwa na mpangilio unaoeleweka wa majira ya mzunguko wa hedhi kwa mwanamke hutokana na kutokuwa na mpangilio sahihi wa homoni. Hii inaweza kufanya wakati halisi wa kushika mimba usijulikane na kupelekea mimba kutotungwa kwa wakati wapenzi wanapo hitaji mtoto.
5. Unene
Mwanamke akiwa na uzito na unene mkubwa anaweza sababisha kutotungwa kwa mimba kutokana uwezekano wa kuzalisha kiwango kikubwa cha homoni oestrojeni inayozuwia mimba kutungwa.
6. Umri
Mwanamke anapofikia umri wa miaka 43, uwezekano wa yeye kushika mimba huwa mdogo. Kwakadri umri wa mwanamke unavyoongezeka na idadi na ubora wa mayai yake hupungua pia.
7. Chakula
Mwanamke anaekosa afya nzuri kutokana na upungufu wa virutubisho mwilini hupunguza uwezekano wa kushika mimba.
8. Madawa
Badhi ya madawa kama yanayotumika kipunguza maumivu na kutibu magonjwa sugu kama kansa yanaweza kusababisha kupungua kwa uwezekano wa mwanamke kushika mimba.
9. Kutoelewa wakati wa kushika mimba
Baadhi ya watu hushindwa kujua wakati sahihi wa mwanamke kushika mimba. Hii hupelekea wapenzi kukutana wakati ambao sio muafaka na kufanya wakakaa muda mrefu bila kupata mtoto.
Wapenzi wanaweza kishi kwa miaka kadhaa kisha wakapata mtoto au wanaweza kuza mwanzo kisha hali ya kutoshika mimba ikajitokeza, moja kati ya sababu hizo inaweza sababiash na sio ajabu.
Inahita kukaa chini mwanake na mwanaume kuona tatizo linaweza kuwa nini, na sio kumwachia mwanmake pekeyake.
Endelea kufuatana nami katika maada mbalimbali au piga simu:
0752674467
0676674467
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni