Jumanne, 21 Februari 2017

Namna ya kumpata mtoto wa kiume au wa kike

Jua namna ya kumpata mtoto wa kiume au wa kike


   Watu wingi wamekuwa wakitamani kupata mtoto wa jinsia fulani kutokana na kupata watoto wa jinsia moja tu. Wengine hutamani mara tu baada ya kuingia katika ndoa wapate mtoto wa jinsia wanayoipenda.

  Iko wazi kuwa kuzaa mtoto wa jinsia fulani ni mpango wa mwenyezi Mungu, lakini mwanadamu amepewa sehemu kidogo sana ya kukamilisha uumbaji. Kwasababu hiyo kukawa na wanasayansi ambao hufunuliwa vitu vichache ili kila mwenye kutaka kujifunza aweze kukamilisha uumbaji wake. Hivo wewe pia unanafasi ya kufanya kitu kwa sehemu fulani kikawa na hujachela.

   Iko wazi kuwa mtu anaweza kupanga na mwenzi wake wazae mtoto wa jinsia gani kwa wakati gani. Kwakuwa sisi wanadamu sio waumbaji, hili huwa ni kwa uwezekano (probability) na ukiwa makini kabisa kunakuwa na uwezekano mkubwa sana wa kupata kile ulicho hitaji kuliko vinginevyo.


   Ili kujua namna ya kupata mtoto wa jinsia fulani, unatakiwa kwanza kujua niwakati gani unaweza kupata mtoto.

   Soma kwa makini mchoro hapo chini kisha ufuatane nami katika maelezo yanayo fuata.

   Wakati wa kushika ujauzito


   Mzunguko wa hedhi ya mwanamke iliyo sawia hukamilika kwa siku 28. Kwa kawaida wanawake wengi huwa na hedhi yenye mzunguko wa siku 28 hadi 32, ingawa wapo wengine huwa na mzunguko mfupi wa siku 14 hadi 25 na wengine mrefu zaidi hadi kufikia siku 42.

   Hapa tutaongelea mtu mwenye mzunguko wa siku 28.

   Siku ya kwanza huanza kuhesabiwa pale tu mwanamke anapoingia hedhi, kama ameingia tarehe 8 basi tarehe hiyo itakuwa siku ya kwanza ya mzunguko wake, na mzunguko wake utaisha pale atapoingia hedhi inayofuata.

   Mfano, akiingia tarehe 8 mwezi wa tano na kuingia tena tarehe 6 mwezi wa sita, basi mzunguko wake utakuwa una siku 29. Kumbuka siku ya kwanza kuingia hedhi ya mwezi unaofuata haihesabiwi katika mzunguko ulionao kwa wakati huo, huhesabiwa kama siku ya kwanza ya mzunguko unaofuata.

   Mwanamke anaweza kuingia hedhi na siku ya tano akatoka, siku ya Kumi na moja ndipo uwezekano wa kushika mimba huanza kuwa. Hii ni kutokana na kukomaa kwa yai lake na kuwa pevu na hutalajia kutoka katika ovari.

   Wastani wa siku anayoingia katika mwezi mpevu (ovulation) ni siku ya 14. Yai hili huweza kukaa masaa 12 hadi 24, baada ya hapo hufunga na kuto kuruhusu urutubishaji.

  Mbegu za mwanaume huweza kukaa hadi siku tatu tangu kuingia katika via vya uzazi vya mwanamke, baada ya hapo huharibika. Kutokana na hilo mwanamke anae tarajia kuingia mwezi mpevu siku ya 13 au 14 akikutana na mwanaume siku ya 11 au 12 anaweza kushika mimba.

   Mwanamke aliyeingia mwezi mpevu siku ya 14 au 15 akikutana na mwanaume siku ya 15 au 16 anaweza kushika mimba.

   Mwanamke akikutana na mwanaume siku ya 14 huwa na uwezekano mkubwa sana wa kushika mimba. Uwezekano wa kushika mimba huongezeka kutoka siku ya 11 hadi 14, na huanza kupungua tena kutoka siku hiyo hadi ya 16.

   Uwezekano wa kushika mimba siku ya 1 hadi ya 10 huwa mdogo mno, kuanzia siku ya 17 hadi 28 pia uwezekano huwa mdogo mno. Mimba inapotokea katika vipindi hivo huwa kuna sababu nyingine zinazo pelekea.


Namna ya kumpata mtoto wa kike


   Anza rasmi kukutana na mpenzi wako siku ya 11 na 12. Katika siku ya 11 anza kuweka mbegu hata mara moja tu au mara mbili, ui pizi maranyingi sana acha nafasi ukutane nae siku ya 12.

   Baada ya hapo mwache ili akiingia mwezi mpevu, yai lake likutane na mbegu zilizo himili kuendelea kuwepo ambazo huwa x, hizo huishi muda mrufu na kuvumilia hali na ndizo husababisha mtoto wa kike.

Namna ya kumpata mtoto wa kiume


   Nivema kukutana usiku wa kuamkia siku ya 14 na siku ya 14 yenyewe. Pia ukikutana nae siku ya 15 au 16 ikawa yai lake bado halijafunga, unaweza kupata mtoto wa kiume.

   Hii ni kutokana na mbegu za kiume kuwa na wepesi wa kuenda na kukutana na yai lililo tayari pevu. Yai linapokuwa tayari mbegu y huwa na uwezekano mkubwa sana wa kurutubisha yai hilo na kusabisha mtoto wa kiume.

   Kutokana na mbegu hizi kutokuwa na ustahimilivu wa hali, hakikisha unakutana na mwanamke ambaye yuko vizuri kisaikolijia, anaefurahia tendo la ndoa. Upatikane muda mrefu wa kumuandaa ili azalishe ute mwingi utakao saidia mbegu kusafiri kwa wepesi na usalama mpaka katika mirija ya folopia ambako urututushaji hufanyikia.

   Sio mbegu zote zinazoweza kufika katika eneo la urutubishaji nyingi hufia nyiani, ni chache na nyingi huwa za kikehasa pale mazingira yapokuwa si mazuri. Za kiume huwa hodari zaidi mazingira yanapo kuwa mazuri ingawa maisha yake huwa mafupi.

NB: Uwezekano wa kupata mtoto wa kiume au wa kike huwa kwa mwanaume, yeye ndo anaweza sababisha mabadiliko yoyote ingawa mwanamke mwenye ushirikiano mzuri kwa mwanaume humwongezea mwanaume uwezekano wa kumpata mtoto anaemtaka.


Endelea kufuatana nami, au piga simu
0752674467
0676674467
 ibrahimmamboleo09@gmail.com

Maoni 1 :

  1. Ikitokea nimefanya tendo siku ya 12 nikija kurudia sikuile ya 14 yenyewe siwezi pata wakiume . Natamani kujua hapo

    JibuFuta